Profesa Jay Anafaa Kuitwa Mkongwe Katika Huu Muziki;-Roma
Msanii wa hip-hop nchini, Roma amefunguka na kusema kuwa katika wasanii anaona wanafaa kuitwa wa kongwe kwake anaona kuwa ni Profesa Jay kwa sababi ndio anafanya vizuri na kupigania sana haki za wasanii kwa kipindi kirefu sana.
Roma amesema kuwa hata kipindi anaanza muziki mpaka sasa, msanii ambae kwake ni role model ni Profesa Jay na wala sio mwingine kwa sababu amekuwa mfano wa kuigwa katika hilo.
Profesa jay anafaa kuwa mkongwe kwenye huu muziki, kwa sababu ni miongoni mwa wasanii waliopigania sana huu muziki kwangu mimi profesa jay ndio role model wangu.