Q-Chief Anazingua :-Juma Nature
Msanii mkongwe wa muziki Juma Nature amerudi tena baada ya miaka kama mitatu mfululizo aliyokaa kimya na kuamu akutoa wimbo wake mpya.
Juma Nature ameachia nyimbo mbili kwa mfululizo lakini amesema kuwa pamoja na kwamba hata yeye maekaa kimya ka muda lakini hawezi kuacha muziki kama alivyofanya Q-chief kwa sababu kila kitu ni swala la kujipanga.
mimi nilimsikia q-chief akiongea lakin niligundua kuwa alikuwa akizingua tu,mtu ambae anafanya vizuri kwa miaka yote hiyo hawezi kuacha muziki kwa namna hiyo , labda unaweza kukaa kimya kwa miaka kutokana na mambo fulani fulani kisha ukarudi ukajipanga.
Juma nanture anasema kwa sasa yuko kwa ajili ya kazi na yupotayari kufanya kazi na kundi lolote la muziki kama ilivyokuwa kwa TMK.