Q-Chillah Aingilia Ugomvi Wa T. I.D na Chid Benz.

Msanii mkongwe wa Bongo Fleva Q-Chillah ameingilia ugomvi unaoendelea kati ya msanii Chid Benz na msanii mwenzyie T.I.D.Wawili hao walijikuta wakiwa katika marubano mazito baada ya msanii T.I.D  kumtuhumu Chid Benz kuwa hafai kusaidiwa,  na tabia yake ya utumiaji wa madawa ya kulevya haiwezi kuisha. Wiki  iliyopita T.I.D alipokuwa anahojiwa katika eNews ya Clouds tv alisema kuwa  ili Chid Benz  aweze kusaidika basi inabidi apelekwe dentention akiwa amefungwa pingu akitulia afunguliwe  akaendelee na muziki wake.

Katika kujibu maneno ya T.I.D , Chid Benz alisema kuwa maneno aliyoyasema T.I.D  ni unafiki kwa sababu yeye anachojua T.I.D ni rafiki yake na kama ameweza kuongea maneno hayo basi T.I.D  ni mnafiki.Kwa mujibu wa Chid Benz yeye ni T.I.D ni marafiki walishafikia hatua ya kushare mpaka magari na T.I.D alikuwa akilala nyumbani kwao .

download latest music    

Akiwa kama rafiki wa karibu wa wasanii wote wawili ,msanii Q-Chillah  ameamua kuongea kuhusu ugomvi huo na kusema “Chid na T.I.D wapo kwenye same situation,wote wanahitaji msaada,tofauti ya Chid na T.I.D ni kwamba Chid anafanya open sana  alafu T.I.D haonekani,kwaiyo wote waache kurushiana maneno wanahitaji msaada”

“Hayo wanayoyafanya ni mambo ya kike,kurudishana maneno ya kwenye khanga” ameongezea Q-Chillah

Katika mahojiano hayo yaliyofanywa na kituo cha Clouds Tv kipindi cha eNews , Q-Chillah amesema kuwa hata alipojitolea kumsaidia kuna baadhi ya watu walisema na yeye anarudi kulekule “Nilijitoa kumsaidia  Chid Benz,lakini baadhi ya watu wakasema na mimi narudi kulekule, nilimsaidia kwa sababu nilihisi kuna siku na yeye atanisaidia mimi. nilijitolea kama kaka,kama rafiki, na ipo siku na yeye atasaidia wengine ”

Kwa muda sasa kumekuwa na kurushiana kwa maneno kati ya wasanii hao   huku T.I.D akionekana kama kuponda Chid Benz, hata hivyo kwa muda sasa Chid amerudi katika game la musiki na kutoa wimbo wake aliomshirikisha Q-Chillah unaojulikana kwa jina la “Muda” ambao pia umekuwa ukifanya vizuri katika vituo mbalimbali  vya Tv na Radio.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.