Queen Darleen Amuomba Msamaha Baba Yake Ili Kukwepa Laana

Msanii wa Muziki wa Bongo fleva kutoka WCB, Mwanahamisi Abdul maarufu kama Queen Darleen amedaiwa kumuangukia kwa magoti Baba yake Mzee Abdul baada ya kuwa bifu la muda mrefu.

Sintofahamu kati ya Baba Diamond na mwanaye ilianza baada ya Queen Darleen kutoa kauli kuwa baba yake ni Diamond Platnumz na kudai Mzee Abdul sio Baba yake Tena.

download latest music    

Global Publishers wanaripoti ili kukwepa laana ya mzazi, hati­maye  Queen Darleen ametambua umuhimu wa wazazi na kuamua kumfuata na kumuomba msa­maha Baba yake.

Kwenye mahojiano na Global Publishers Baba Diamond amesema ni kweli awali ali­kuwa na ugomvi mkub­wa na Queen Darleen na ikafikia hatua mpaka ya kumtamkia maneno mazito kuwa hata akifa binti yake huyo asimzike ila anamshukuru Mungu kwamba mwanaye huyo ametambua makosa yake na kujirudi.

Haya ni mambo ya kawaida tu katika familia, ni kweli mimi na Queen Darleen tulikuwa na ugomvi mkubwa mpaka ikafikia hatua nikamtamkia maneno mabaya kwamba iki­tokea nimefariki dunia asije kunizika, jambo ambalo si zuri, lakini ameyatambua ma­kosa yake, akaja kuniomba msa­maha na mimi nikamsamehe kwa moyo mmoja”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.