Rafiki Yako Akikusaliti Tupa Kule Usithubutu Kuwa Naye Karibu- Ray C

Mwanamuziki mkongwe wa Bongo fleva Rehema Chalamila ‘Ray C’ Kiuno bila mfupa amefunguka na kuwapa ushauri mashabiki zake kuwa endapo kuna rafiki yako amekusaliti achana naye.

Ray C ambaye hapo nyuma amewahi kufunguka kuhusiana na usaliti uliopata mara baada ya kuingia kwenye matumizi ya madawa ya kulevya ambapo alifunguka kuwa watu wote aliodhani kuwa ni marafiki zake walimsaliti na alibaki amesimama mwenyewe.

download latest music    

Ray C ametumia ukurasa wake wa Instagram kufikisha ujumbe huo ambao ameonyesha pia unamhusu na yeye:

Ukiona rafiki kakugeuka, usije thubutu kuwa naye karibu tena huyo ni zaidi ya nyoka. Tena bora Nyoka ukikutana naye harembi kujifanyisha mzuri kwako, anakugonga tu fasta kabla hujamdhuru kuliko huyo anayejifanya kwako mzuri na ukiondoka tu anakung’ong’a”.

Ray C alisindikiza ujumbe huo kwa neno Chefu si kidogo. Hivi sasa Ray c anatamba na wimbo wake Rudi Kidogo na anafanya sana matamsha yake nje ya nchi kama Kenya, South Africa na kwingineko.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.