Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta na wasanii kutoka Kenya watuma salamu za rambirambi kufuatia vifo vya wanafunzi 32 Arusha

Image: epa03891049 Kenyan President Uhuru Kenyatta attends an inter-faith prayers ceremony held for the victims of the Westgate shopping mall terrorist attack in Nairobi, Kenya, 01 October 2013. Kenyatta vowed that the military will continue its operations in Somalia. EPA/DAI KUROKAWA

Wakenya wametumama salamu za rambirambi kufuatia vifo vya wanafunzi 32, walimu 2 na dereva walifariki baada ya gari walilokuwa wakisafiria kutumbukia korongoni kwenye eneo la Rhotia wilayani Karatu.

Wanafunzi na walimu hao walikuwa wanaenda kwenye shule iitwayo Tumaini kwa ajili ya kufanya mitihani wa ujirani mwema.

download latest music    

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta and wasanii kadhaa wametumama salamu za rambirambi kufuatia vifo vya wanafunzi na walimu hao.

Uhuru Kenyatta – Rais wa Kenya

Rais Kenyatta alituma pole kwa Rais John Magufuli alipokuwa akifanya kampeni zake, aliomba watu wasimame kwa dakika moja kuomboleza wanafunzi walioaga.

Mzazi Willy Tuva – Radio presenter radio Citizen

Tunaungana na ndugu na dada zetu wa Tanzania kwa Msiba uliowasibu Jumamosi kwenye ajali iliyotokea Arusha na kusababisha vifo vya wanafunzi 32, walimu wawili na dereva wao .

Mola wape nguvu wazazi, ndugu, dada, jamaa, marafiki na Watanzania wote na tuwaombee waliotuacha .

Inauma sana. Inatia majonzi sana. Tanzania hamko peke yenu, tuko pamoja wakati huu mgumu .

#TanzaniaTukoPamoja

Bahati – mwimbaji wa nyimbo za Injili

REST IN PEACE ? Just to send my condolences to Our Neighbour’s Tanzania Wamewapoteza Watoto 32 Wa Primary School kwa ajali mbaya ya Gari la Shule huko ARUSHA… We pray for Strength kwa Family zote Waliowapoteza Wapendwa. Mungu awalaze Mahali Pema!

Nyota Ndogo – mwimbaji

Mimi sina raha kabisa yani hata sioni nikiposti kitu chengine MUNGU wangu waeke pema peponi.wazazi wanalia mpaka nami nalia yani mpaka uzazi unaniiuma.watanzania poleni sana

Nameless – mwimbaji

My condolences to my brothers and sisters in Tanzania for the loss. Mola na awalaze pema watoto wetu.

#TutaonanaBaadaye

Mercy Masika – mwimbaji wa nyimbo za Injili

The loss of a child can never be replaced but our hope is in the knowledge of the one who holds our lives. Poleni sana Tanzania. Mungu anayajua haya na awape amani kwa hiki kipindi kigumu kwa wazazi marafiki na nchi yote .

Pole zetu ziwafikie , Mungu ana mpango mzuri na ni salama kwetu sababu yu hai . Amani . Arusha st vincent #MunguMfarijiWetu #RIP WATOTO WA TANZANIA.

 

 

 

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere