Rammy Galis Kumkatia Fungu La Pesa Mtoto wa Masogange

Muigizaji wa Bongo movie Rammy Galis ambaye alijizolea umaarufu kipindi cha nyuma baada ya kuwa Kwenye uhusiano wa kimapenzi na Marehemu Agnes Gerald ‘Masogange’.

Rammy Galis amefunguka na kudai kuwa amekusudia kumpa fungu la pesa Sania ambaye ni mtoto wa Marehemu Agnes mara baada ya kuzindua filamu aliyoigiza naye.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Planet Bongo ya East Africa Radio, Rammy amesema atahakikisha fungu hilo la pesa atamkabidhi mtoto Sania mwenyewe kutokana na kazi aliyofanya mama yake kwenye filamu hiyo:

Kwanza nisingependa kutangaza rasmi kiasi ambacho kitamfikia kwa sababu sijui filamu mauzo yake yatakuaje lakini mimi kama Rammy galis nitatoa kile ambacho Mungu atanibariki katika filamu hii, kutakuwa na asilimia kadhaa ambayo nitaiweka kwa niaba ya mtoto”.

Lakini pia Rammy Galis ameweka wazi kuwa anasubiri Kwanza muda upite ili watu wasahau machungu ya msiba ndipo akafanye uzinduzi maana asije akaambiwa anatafuta kiki.

Agnes Masogange aliaga dunia wiki chache zilizopita baada ya kuugua ghafla.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.