Ray C Amuomba Raisi Magufuli Apitishe Sheria Ya Mpya Kuhusu Ndoa

Mwanamuziki mkongwe wa Bongo fleva Rehema Chalamila au maarufu kama Ray C ameibuka na kumuomba Raisi Magufuli kupitisha sheria iyakayoangalia mahusiano ya kimapenzi kati ya mwanamke na mwanaume.

Ray C alifunguka haya kupitia ukurasa wake wa Instagram siku ya jana ambapo aliweka picha ya Raisi John Pombe Magufuli na kumuomba ahahakikishe kuwa Tanzania kuna kuwa na sheria ambayo itahahakikisha kuwa mwanaume na mwanamke wasiwe na mahusiano ya kimapenzi hadi pale watakapofunga ndoa ili wanawake wengi wapate nafasi ya kuolewa.

download latest music    

Ray C amefunguka hayo kwa kile alichodai kuwa wanaume wengi wana tabia ya kuchezea wasichana na wa watu na mwisho wake wanawaacha solemba bila ndoa na badala yake wanaishia kuoa wasichana wengine.

Ray C aliandiika maneno haya machache katika ukurasa wake wa Instagram:

Mzee mimi nina shida moja hawa wanaume hapa nchini wanajifanya wajuaji sana! ombi langu kwako kwa mwaka huu ni hili! Naomba upitishe sheria kama ya Sultan Qaboos wa Oman! Hakuna mahusiano kati ya mwanamke na mwanaume mpaka pale watakapofunga ndoa. Na yeyote atakayekutwa na mwanamke iwe hotelini au guest house bila cheti cha ndoa wapelekwe wote segerea. Nadhani itasaidia sana kwani wanawake wengi wataolewa badala ya kuishia kuwa manungayembe! Utakuwa umewanyoosha sana hawa wanaume wetu nadhani tutaweza kuheshimiana”.

Ray C ameongea hayo kuhusu ndoa na mahusiano ingawa yeye binafsi alishaweka wazi kipindi cha nyuma kidogo kiwa kwa sasa hana mahusiano ya kimapenzi na mwanaume yoyote kwani mahusiano ya kimapenzi  yamesha mpotezea sana muda wake kipindi cha nyuma.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.