Ray C ashindwa kuficha furaha yake baada ya Diamond kukiri hili

Rehema Chalamila maarufu kama Ray C ameishiwa na maneno ya kusema baada ya Diamond Platnumz kufunguka kuhusu nia yake kimuziki.

Diamond alisema nia yake ni kuinua wasanii wengi kumuziki kwani wao kama yeye wamelelewa kwa umaskini. Super star huyo alisema hayo akitangaza uzidunzi wa msanii mpya wa Wasafi.

download latest music    

“Panapo majaaliwa siku ya jumatatu kesho, ntakuwepo kwenye LEO TENA ya Clouds fm na familia nzima ya @Wcb_wasafi tukimtambulisha Kijana mwenzetu Mwingine Mpya toka Mtaani, ndani ya @Wcb_Wasafi….. Sisi ni vijana ambao tumekulia kwenye umaskini na bado tupo kwenye kupambana namna ya kujikwamua kwenye umasikini… na ndiomaana tunajitahidi kadri ya uwezo wetu kila tukiona kijana yoyote mwenye nia na kipaji kumsaidia kwa kadri ya uwezo wetu, ili nae aweze kutambulisha kazi zake, na Pengine Mwenyez Mungu akimjaalia nae awe mkombozi kwenye Familia yake….Sio jambo Rahisi ni gumu, lakini kwa Sapoti yenu naamini tunaweza lifanikisha…Siku zote naomba mkumbuke WCB_Wasafi sio ya Diamond, ni ya vijana wote wapambanaji…na ndiomaana kila siku nawaomba Muendelee kuniombea na Kunisapoti, kwani Sapoti yenu ndio itayo nifanya hata kesho niweze kukuchukua wewe ama ndugu yako ili aje kukitambulisha kipaji chake na Mwenyez Mungu akijaalia kufikia Malengo…… USIKOSE kusikiliza Leo tena ya @Cloudsfmtz saa nne Asubuhi…Shukran?” Diamond aliandika kwa Instagram.

Ray C alifurahiswa na maneno ya Diamond kwa kiasi kwamba akaamua kumsifu kwenye mitendao ya kijamii. Alisema roho ya Diamond hauna ubinafsi kabisa.

“Wakitokea wasanii wakubwa kama wewe na wakawa na moyo kama wako basi muziki wetu utafika mbali sana…Kaa na huyu kijana japo nusu Saa tu,utaelewa kwa nini nasema haya!!Kuna Ro!!!!Na kuna RoHo!!!Jamaa ana Roho ya Peke Yake Maskini!!!!Na Mengi Moyoni natamani niongee lakini Haya Yanatosha mdogo wangu!!Kumbuka Mwenye Hii Dunia alishasema ,Mtoaji hupewa Zaid na Zaid…… Mungu akutangulie katika kila ufanyalo Inshallah…” Alisema Ray C.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere