Ray C na Rostam Wala Shavu Kutoka Kwa Msanii Wa Kenya

Raper wa muziki kutoka Kenya Khaligraph Jones siku ya jana aliachia rasmi albamu yake.

Albamu hiyo aliyoipa jina la Testimony 1990 ina nyimbo zipatazo kumi na saba na habari njema ni kwamba ndani ya nyimbo hizo kuna wasanii watatu wa Bongo fleva walioweka mkono humo.

download latest music    

Wasanii wa Bongo fleva ambao watasikika Kwenye Albamu hiyo ni pamoja na Msanii mkongwe wa Bongo fleva Rehema Chalamila ‘Ray c’ aliyeimba wimbo unaoitwa ‘Aisee’ na kundi la Rostam linalounda na Stamina na Roma.

Roma na Stamina watasikika katika albamu hiyo Kupitia kibao chao cha ‘Now you know’.

Hii inaonyesha ni jinsi gani muziki wetu wa Bongo fleva unavyozidi kukua kila siku na hata kufika kabisa mbele na kimataifa zaidi.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.