Rayvanny Afungukia Suala la Rich Mavoko Kutimuliwa WCB

Staa wa muziki wa Bongo fleva kutoka katika label ya WCB, Rayvanny amefunguka kuhusu Tetesi za Msanii mwenzake Rich Mavoko kutimuliwa kutoka katika label hiyo.

Tetesi za Mavoko kutimuliwa WCB zilianza kusambaa mwezi uliopita baada ya kutoonekana Kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanywa na WCB ambao ulijumuisha wasanii wote wa label Lakini pia Mavoko hajaonekana Kwenye trailer ya shoo mpya ya Wasafi.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Wasafi Tv, Rayvanny amesema hawezi kuliongelea sana suala hilo kwa sababu sio msemaji lakini amesema Rich Mavoko bado yupo na huwa wanawasiliana naye mara kwa mara:

Ujue sisi tunachekiwa kwenye group, leo kuna tukio hili na hili, so ukiona huyo kakosa ni masuala ya uongozi sana labda angekuwepo Diamond au Babu Tale angeweza kuongea sana lakini Mavoko yupo Wasafi kila siku.

Anakuja, anajiunga kwenye vitu lakini yeye kutokuja siku ile sijui sababu, kama kuna vitu vinavyoendelea ni yeye na uongozi. Mimi siwezi kuongea sana kwa sababu Mavoko ni mwanangu tunaongea tunachati, tunarekodi ngoma zetu“.

Lakini Hata hiyo Babu Tale alieleza kuwa siku hiyo Rich Mavoko alikuwa aki-shoot video ya wimbo wake mpya na kushindwa kuhudhuria.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.