Rayvanny Ahofia Kuibiwa Mpenzi Wake na Wanaume Wakware

Mwanamuziki wa Bongo fleva anayefanya vizuri hivi sasa kutoka WCB, Rayvanny amefunguka na kuweka wazi kuwa anahofia wanaume wakware washiriki wakamuiba mpenzi wake Fahyma.

Siku za hivi karibuni Rayvanny amekuwa akiwa mstari wa mbele kujulisha watu wote kuwa anampenda mpenzi wake Fahyma kwani amekuwa akimposti mara kwa mara kwenye ukurasa wake wa Instagram.

download latest music    

Hata ni siku chache tu zilizopita ambapo Rayvanny aliweka wazi mipango yake ya kutaka kumuoa mpenzi wake baada ya kuandika kwamba hivi karibuni atamchukua jumla jumla mrembo ambaye amemzalisha mtoto mmoja, Jayden.

Jana Kupitia ukurasa wake Instagram Rayvanny amemtahadharisha mpenzi wake juu ya kuwa makini na wanaume wakware ambao watajaribu kumtongoza na kuharibu penzi lao:

Itaniuma sana siku Pumbavu wakiniibia…..Mama jilinde ukipewa hi tu wewe Buloooock……..maana wanaanziaga mahali”.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.