“Rayvanny Alivyofungiwa Nilikuwa Napata Mawazo Sana”- Fahyma

Mpenzi na mama Watoto wa staa wa Bongo fleva kutoka katika label ya WCB Rayvanny, Fahyma ‘ Fahyvanny’ amefunguka na kuweka wazi Furaha yake Baada ya Rayvanny kufunguliwa na BASATA.

Fahyma amekiri kufurahishwa na kitendo cha baba mtoto wake huyo kusamehewa na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) kwani ishu hiyo ilikuwa inamnyima usingizi.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa, Fahyma alisema katika kitu kilichokuwa kinampa mawazo na kukosa kabisa usingizi ni kufungiwa kwa baba mtoto wake huyo lakini kwa sasa anaishukuru Basata kwa kuwahurumia na kuwafungulia kuendelea na kazi kama kawaida.

Kufungiwa kwa Rayvanny kulikuwa kunanipa mawazo sana maana nilikuwa nawaza maisha yetu yatakuwaje na tulikuwa hatujui msamaha utatoka lini lakini tunashukuru Mungu wamesamehewa na mwisho wa siku maisha mengine yanaendelea, nitaendelea kumhimiza asirudie kosa tena”.

Rayvanny na Diamond Platnumz walifungiwa na BASATA Baada ya kupandishwa stejini na kuperfom wimbo wao wa ‘Mwanza’ ambao ulikuwa umepigwa stop kwa kukiuka maadili ya Kitanzania.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.