Rayvanny Amwagia Povu Zito Dogo Janja

Staa wa muziki wa Bongo fleva kutoka label ya WCB Rayvanny amemwagia povu zito msanii mwenzake Dogo Janja na kumtaka ampe heshima yake.

Siku chache zilizopita Dogo Janja alimtaja Rayvanny kama msanii ambaye hajui kuvaa Kwenye Interview yake na Wasafi Tv na kujitolea kumvalisha.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Wasafi Tv, Rayvanny amejibu tuhuma hizo na kusema kuwa Dogo Janja anakosea kusema hivyo kuni kuna tofauti kati ya mtu kujua kuvaa na mtu kupendeza.

Kuna tofauti kati ya kuvaa na kupendeza, mtu akikuambia hujui kuvaa, anakosea, labda akuambie hujui kupendeza.

Cheni yake ambayo anaivaa sasa hivi, aliivaa Dully Sykes kwenye wimbo wa Sugar Mami. Kwa hiyo ukija kusema eti una uwezo wa kumvalisha Rayvanny hajui kuvaa, no!, unanikosea heshima kwa sababu mimi nimeenda sehemu nyingi nimeona watu wanavaa vitu tofauti”.

Dogo Janja ameendelea kufanya vizuri na ngoma yake mpya ya ‘Banana’ ambayo imeendelea kushika namba moja Kwenye mtandao wa YouTube.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.