Rayvanny Athibitisha Kuwa Sababu ya Kusainiwa kwa Mboso WCB

Msanii Rayvanny amefunguka kuwa aliwahi kumshawishi Diamond Platnumz kumsaidi Mbosso ndani ya WCB, Kipindi hicho ambacho msanii huyo alikuwa bado hajasainiwa sehemu yoyote baada ya kutoka Ya Moto band,

Rayvanny amefunguka hayo alipoulizwa anajisikiaje wimbo ‘Jibebe’ ndio ameandaliwa Challenge badala ya wimbo wake Chombo ambao ndio ulikuwa kwenye mipango hiyo hapo awali. “Mbosso Lava Lava ni watu ambao walinikuta Wasafi na pia nilikuwa nawaambia msikate tamaa kila kitu kinaenda sawa. Na nilikuwa naongea na Diamond bhana Mbosso yupo vizuri lakini hana Management  tumsaidiae, mimi ndio nimelazimisha hadi Mbosso amefika pale,” amesema Rayvvnny.

download latest music    

Kabla ya Mbosso kuingia WCB alikuwa akifanya vizuri na kundi la Yamoto Band, wakati Rayvanny kabla ya kusainiwa kwenye lebo hiyo alikuwa Tip Top Connection ingawa hakupata nafasi ya kusikika sana

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.