Rayvanny na Fayma Kufunga Ndoa.
Msanii wa muziki kutoka lebel ya WCB Rayvanny ametangaza kufunga ndoa na mzazi mwenzie ambae pia ni mpenzi wake wa siku nyingi fayma .
Rayvanny anaweza kuwa msani wa kwanza kutoka katika lebel hiyo Kutangaza kufunga ndoa na kama ndoa hiyo itakamilika basi pia atakuwa msanii wa kwanza kufunga ndoa na kukaa katika mahusiano yaliyodumu na yasiyokuwa na drama katika lebel hiyo.
Siku za nyuma kidogo msanii huyo aliwahi kuweka oicha nyingi zikimuonyesha akiwa amekwenda nyumbani kwao Mbeya ambapo alikwenda kumtambulisha mpenzi wake huyo na mtoto wao wa kiume.