Rc Makonda Amtetea Wema Kuwa Tanzania Sweetheart Amtaka Mobetto Awe Buguruni Sweetheart
Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam, Mh. Paul Makonda ameibuka na kumkingia kifua Muigizaji wa Bongo movie Wema Sepetu na kusema analistahili Jina la Tanzania Sweetheart na sio Hamisa Mobetto.
Kwa wiki chache zilizopita Wema Sepetu amekuwa akifanya interviews mbali mbali na amekuwa akibainisha kuwa yeye ndiye Tanzania Sweetheart na sio Mobetto kama mashabiki zake ambavyo wamekuwa wakilazimisha.
Siku chache zilizopita akiwa katika Birthday Bash ya Wema iliyofanyika katika viwanja vya Mlimani City, Makonda aliweka wazi kuwa Wema ndiye Tanzania Sweetheart pekee ila kama wengine wanalitaka hilo Jina wanaweza kuwa Buguruni Sweetheart.
Wema ni Tanzania Sweetheart kwa sababu kuna vigezo, na kwanza hujiiti Jina mwenyewe, watu wanakupa Jina kama alivyopewa na Baba yake na mama yake Jina Tanzania Sweetheart wengine wanaweza kuwa Buguruni Sweetheart sio dhambi au Manzese Sweetheart”.
Vita kali ya Jina la Tanzania Sweetheart ilianza baada ya mashabiki Mtandaoni kusema wanamvua Jina hilo Wema na kumpa Mobetto kwa sababu Wena amepoteza umaarufu wake na kuwachukiza mashabiki zake kwa matendo yake ya mitandaoni.