RC Makonda Atangaza Ndoa Ya Majizzo na Lulu

Mkui wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda ametangaza rasmi kuwa Muigizaji wa Bongo movie Lulu Michael na Mkurugenzi wa EFM Majizzo watafunga ndoa hivi karibuni.

Kumekuwa na tetesi nyingi tangu Lulu atoke gerezani wiki chache zilizopita ikiwemo kuwa ni mjamzito na kuwa anatarajia kufunga ndoa na mpenzi wake Majizzo.

download latest music    

Hatimaye Paul Makonda amethibitisha taarifa hizo baada ya kuandika Kwenye mitandao ya kijamii kuwa yeye ni mwenye kati wa shughuli hiyo ambayo itafanyika hivi karibuni lakini hajweza kutaja tarehe.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram RC Makonda kaandika maneno haya:

Nikiwa mwenyekiti wa  kamati ya Harusi ya bwana Majizzo na Bi Elizabeth Michael (Lulu) nimeupitisha huu wimbo wa Mrisho Mpoto na Harmonize kuwa ndio winbo rasmi wa Harusi yao, kuhusu tarehe za harusi endelea kufuatilia 92.5 Dodoma”.

Mpaka sasa Maharusi Watarajiwa hawajathibitisha taarifa hizo.

Lulu alifungwa jela mwaka jana mwishoni baada ya kukutwa na hatia ya kumuua bila kukusudia marehemu Steven Kanumba.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.