RC Makonda Awachana Wabongo Kisa Ommy Dimpoz

Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda ameibuka na kuwajia juu Mashabiki wa muziki wa Bongo fleva ambao wamegoma kuonyesha sapoti kwa muziki wa Ommy Dimpoz Baada ya kuachia wimbo mpya.

RC Makonda akimtolea mfano msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Ommy Dimpoz, amesema kuwa kuna watu kipindi msanii huyo anaugua, walikuwa wanatangaza amefariki dunia, leo amepona na ametoa wimbo wake mpya wa kumshukuru Mungu watu hao wamekaa kimya kama hawajui.

download latest music    

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Makonda ameandika ujumbe huu mzito:

Ukitaka kujua watu walivyo wa Ajabu tazama leo, Ommy dimpo alikuwa mgonjwa sana na ikafika hatua ya watu kutangaza Amekufa. Leo amerejea tena akiwa na wimbo wa kumshukuru Mungu wamekaa kimya Kama vile siyo wao waliokuwa wana post kumwombea apone. Angefariki tungeona mitandao yote imechafuka RIP Ommy oooh umeenda bado tunakuhitaji. Unafiki huu sijuwi utaisha lini, tunapenda kutangaza msiba kuliko Uponyaji”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.