Rich Mavoko Ashindwa Kujizuia Aanika Penzi Lake na Lulu Diva Hadharani

Mwanamuziki wa Bongo fleva kutoka WCB, Rich Mavoko ameshindwa kuzuia hisia zake na kuanika hadharani penzi lake kwa msanii mwenzake Lulu Diva.

Kwa muda mrefu kumekuwa na tetesi kuwa Rich Mavoko anafaidi penzi la Mrembo Lulu Diva ingawa wenyewe wamekataa tetesi hizo mara kwa mara huku wakidai sio wapenzi.

download latest music    

Siku za nyuma Lulu Diva alitakiwa Kuolewa na mwanaume ambaye alikuwa ameshamtolea mahari lakini mahari Ile iliishia kurudishwa huku ikidaiwa sababu kubwa ni Rich Mavoko.

Kama waswahili wanavyosema mapenzi kikohozi basi ndio mahaba yamemzidi Rich Mavoko kwani siku moja baada ya video yao wakibusiana kusambaa Mtandaoni Rich Mavoko kakiri mapenzi yake kwa Lulu Diva.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Rich Mavoko kaandika ujumbe mzito wa kimahaba kwa mpenzi wake Lulu Diva:

Sioni maneno ya watu kwangu kama Choo. Mtoto kama chumvi nilipokuonja nikaomba poo”.

 

 

Baada ya Mavoko kufunguka hayo mazito, Lulu Diva aliachia makopa kibao yakisindikizwa na ujumbe uliosema:

Aaaawwww My Love”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.