Rich Mavoko Atangaza Kuwa na Lebel Yake, Ataja Wasanii Anaotamani Kufanya nao Kazi
Msanii Rich Mavoko amefunguka na kusema kuwa kwa sasa ameanza kujisimamai mwenyewe baada ya kutoka katika kusimamiwa na msanii Diamond Platinumz katika label ya Wasafi na kuachana nayo kwa migogoro hivyo ameamua kufanya kazi mwenyewe.
Akiongea na clouds Media, Rich Mavoko anasema kuwa pamoja na kufanya hivyo alkini pia amekuwa na lebel yake ambayo inasimamiwa na mama yake mzazi na dada yake Dokii na ameanza kutafuta wasanii ambao anaweza kuwasimamia katika uongozi wake.
kwa sasa nimesimama mimi kama mimi sina menejiment yoyote, billionaireskids ni lebel yangu ambayo inasimamiwa na mama yangu na dada yangu dokii ambae yuko kama mshauri wangu.
Hata hivyo Rich amewataja wasanii ambao anatamani kufanya nao kazi katika uongozi wake kuwa ni Foby na Sheby na sasa wapo katika mazungumzo.
Foby na Sheby ni wasanii ninaotamani sana kufanya nao kazi kwa sasa na kama tutakubaliana basi watakuwa wasanii wa kwanza katika lebel ya bilionaireskids.