Rich Mavoko: Mimi na Lulu Diva ni Washkaji Tu

Mwanamuziki mkongwe wa Bongo fleva Rich mavoko ameibuka na kudai kuwa yeye na msanii mwenzake Lulu Diva ni washkaji tu.

Siku chache zilizopita Mavoko na Lulu Diva waliamsha Tetesi za kuwa Kwenye Mahusiano baada ya video iliyowaonyesha wakibusiana kuenea Mtandaoni na baadae Mavoko kumposti Lulu Diva na kumpa maneno matamu.

download latest music    

Lakini baadae ilikuja kujulikana kuwa yalikuwa ni maneno yanayopatikana Kwenye wimbo wao mpya unaojulikana kama Ona ambao kwa hivi sasa inafanya sana pia Kwenye Sehemu mbali mbali.

Siku ya jana Mavoko alihudhuria hafla ya Iftari iliyoandaliwa na Wasafi Tv na alipoulizwa na Dizzim Online kuhusu Lulu Diva ambaye walikuwa wameongozana alidai hawana mahusiano bali marafiki wazuri tu.

Mimi Lulu Diva ni kama washkaji tu kwaiyo kwa ajili ya urafiki wetu tuliamua kufanya kazi pamoja na ndio ile mnayoiona nyimbo inaitwa Ona, na alivyokuja kwangu alikuja kibiashara na alipitia Kwenye management kila kitu kwaiyo unaweza ukaona kabisa siyo  demu wangu na wala sina mahusiano naye zaidi ya urafiki”.

Kuna tetesi zinazodai kuwa Lulu Diva alimuacha mpenzi wake aliyekuwa amemchumbia na aliyekuwa tayari kumuoa kwa ajili ya penzi la Mavoko.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.