Rich Mavoko na Diamond Wakutana BASATA Uso kwa Uso

Msanii wa Bongo Fleva, Rich Mavoko na lebo ya WCB wamekutana tena Baraza la Sanaa Taifa (BASATA).
Team ya WCB ilikuwa ikiongozwa na Diamond Platnumz pamoja na Sallam SK.
Pande hizo mbili ziliitwa na BASATA kwa lengo la majadiliano mara ya baada ya upande wa Rich Mavoko kulalamikia kile walichodai ni mkataba wa unyonyaji kutokea WCB.
Hata hivyo hadi pande zote mbili zinaondoka eneo la BASATA hazijaweka wazi ni kipi hasa kinaeendelea, hivyo wenye kauli ya kueleza yalipofikia mazungumzo hayo ni Baraza hilo lenyewe.
Mavoko alijiunga na WCB mwaka 2016 akisaini chini ya lebo hiyo na kuanza kufanya kazi akiwa chini ya lebo hiyo ambayo boss wake ni Diamond Platinumz.
Baada ya kujiunga na lebo hiyo Mavoko alianza malalamiko mapema mwaka huu kuwa anataka kujitoa katika lebo hiyo ya WCB wasafi kwa madai kwamba ananyonywa kimaslahi.
Mbali na kunyonywa kimaslahi lakini pia ilidaiwa kuwa kuna vitu ndani ya makataba huo msanii huyo hakutimiziwa na boss wake kama mkataba ulikuwa unaelekeza.
Malalamiko ya Mavoko yalionekana kuwagusa wengi na ikachangia Mavoko kukaa kimya kwa muda ingawa siku za hivi karibuni aliachia ngama yake mpya inayokwenda kwa jina la Ndegele.
Katika moja ya mahojiano aliyofanya meneja wa Diamond Salam Sk katika moja ya Redio hapa nchini alipoulizwa kuhusiana na madai haya ya mavoko alisema “Mavoko bado ni msanii wa WCB na hayo malalamiko anayotoa sisi hatujui yanahusiana na nini kwani huduma zote wanazopatiwa wasanii wa WCB anazipata”
Meneja huyo aliongeza “Kabla ya mavokonkusaini mkataba alipewa akakae nao aupitie hadi ajirizishe na Mavoko alifanya hivyo na kukaa nao ndani ya wiki mbili ndio akaurizia mwisho wa siku akaja kusaini sasa anacholalamika ni nini? sisi hatujui kwani makataba huo una kurasa 10 kwahiyo hatujui ni kitu gani anataka haswa”
Baada ya Mavoko kupeleka malalamiko hayo Basata,Basata nao waliamua kuwaita Maboss wa WCB walipofika wakaongea nao na ndio wakakubaliana wakutane siku ya leo August 23 katika ofisi hizo hapa Jijini Dar Es Salaam.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.