Roma aweka wazi kuwa amewasamehea na kuwasahau waliohusika na kutekwa kwani

Roma ambaye ni msanii wa hiphop bongo alitekwa miezi kadhaa iliyopita lakini akapatikana baada ya siku kadhaa kitu ambacho yeye Kama mwanadamu hajaweza kusahau.

Hivi karibuni akizungumza na Times FM, Roma alifunguka kudai kuwa tangu awachiliwe serikali ya Tanzania haikumsaidia kwa njia yoyote. Msanii huyu alisema kuwa familia, marafiki na mashabiki ndio walisimama na yeye hadi kupona kwake. Alipoulizwa ikiwa Serikali ilimjulia hali wala kumshughulikia alijibu kwa kusema,

download latest music    

“Lahashaa! Hapana juu kwa juu tuu polisi, polisi Mwananyamala PF3 sijui nini ile, baada ya pale nikajiongoza mimi mwenyewe na familia yangu,so ikawa hivyo tuu“

Hata hivyo Roma alisema kuwa ameshawasamehe na amewasahau wote waliohusika na kutekwa kwake.

“Yaliyopita yamepita tunasamehe,tunasahau waliohusika Mungu atawahukumu na mkono wake na Mungu atupe neema uvumilivu na neema ya kuwasamehe…Lakini usidanganyike na mtu anakwambia sijui alikuja akatoa bugana lake au sijui akatoa hela ya panadol, Lahashaa!“

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua