Roma Mkatoliki arejelea kazi yake ya ualimu

Watu wengi hawakua wanajua kazi aliyokuwa akifanya Roma Mkatoliki kabla ya kujiunga na sanaa. Rapa huyo anarudi shuleni kwa muda mfupi.

Roma alikua mwalimu wa somo la Hisabati kabla ya kuamua kuanza kuangusha mistari kwa ngoma zake za kuvutia.

download latest music    

Rapa huyo alienda kufunza hisabati katika shule ya msingi ya Mchikichini iliyopo Mbagala-Kibondemaji jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Showbiz Xtra kabla ya kuelekea shuleni, Roma alisema kuwa ameamua kuchukua nafasi hiyo kwanza kujikumbushia kazi yake ya ualimu.

“Somo la hisabati ni miongoni mwa masomo yanayotengwa sana na wanafunzi wengi hivyo basi nikiwa kama mwalimu niliyepitia kufundisha somo hili, nimeona vyema kuhamasisha wanafunzi walipende na kuliamini. Nitagawa vitabu vya hesabu kwa wanafunzi wa darasa la saba na pia kuwafundisha somo hilo. Kila mmoja nitahakikisha amehamasika na somo hili na kulipenda kama masomo mengine,” alisema Roma.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere