Rosa Ree Afunguka Kuhusu Kuondoka Kwenye Label Ya The Industry

Mwanamuziki wa bongo fleva anayefanya miondoko ya rap, Rosa Ree amefunguka na kukubali kuwa tetesi zilizoenea kuwa yeye ameachana na label ya The Industry ni kweli.

Label ya The Industry ambayo inasimamiwa na wanamuziki kutoka Navy Kenzo Nahreel na Aika iliyokuwa inasimamia kazi za mwanadada Rosa Ree ambaye amepata umaarufu kutokana na staili yake tofauti na wasanii wengine ya kuimba kwa kurap huku watu wengi wakimfananisha na rapa maarufu kutoka Marekani mwanadada Nicki Minaj.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Millard Ayo Tv, Rosa ree alifunguka zaidi kuhusiana na uamuzi wake wa kuondoka katika label hiyo;

Ni kweli kwa sasa sipo tena kwenye label ya The Industry ila sio kwamba nimeondoka au kuendelea ila ni mkataba umeisha at the moment na tuko salama kabisa ni vitu vya mkataba ni masuala ya biashara haituingilii kwenye urafiki au ufamilia tunaoweza kuwa nao kwaiyo tunaishi kama zamani tupo freshi na bado ni marafiki kwaiyo hamna kitu chochote kibaya kilichotokea kati yetu. Pia napenda kuwashukuru kwa mchango wao ambao wameweza kuweka kwenye mziki wangu kwani sio rahisi watu wakuamini kwaiyo ni kitu ambacho they really deserve credit for na walifanya kwa moyo mmoja kwaiyo nawashukuru kwa hilo “.

Baada ya Rosa Ree kuondoka The Industry hivi karibuni watu wengi walizusha kuwa ameondolewa kwa sababu ya mambo ya kiheshima na pi ailisemekana kuwa Rosa Ree alikuwa na ugomvi na First lady wa The Industry Aikah kitu ambacho wote wamekataa huku akisisitiza kuwa hana ugomvi nao bado ni marafiki kama zamani lakini tu mkataba wake umeisha ila kwa sasa Rosa Ree kasema anajisimamia mwenyewe.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.