Rosa Ree Afunguka ni Sababu Gani Zilimpelekea Kumtosa Fid-Q

Msanii wa kike anayetamba kwa staili ya peke yake ya kuimba na kurap Rosa Ree, amefunguka kuwa ni sababu gani iliyompelekea kumtosa mwanamuzi mkongwe  Fid-Q.

Rosa Ree anayetamba na wimbo wake mpya wa ‘Dow’ amekuwa katika vichwa vya habari hivi karibuni baada ya habari kutapakaa kuwa amehama label ya The Industry ingawa ameendelea kusisitiza kuwa hana shida nao lakini za chini ya kapeti zinadai mengine. Kumekuwa na tetesi nyingi kuwa mkali wa mashairi, Fid-q alipomtaka Rosa Ree wafanye kazi alikataa.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyoyafanya na Lilommy, Rosa Ree amefunguka yafuatayo kuhusiana na masuala hayo:

Naweza kusema wimbo wa Fid-Q ni moja Kati ya vitu ambavyo The Industry imeniangusha sana, nilitumiwa hiyo nyimbo na nikaandika mpaka verse lakini ikawa inatakiwa ipite kwanza kwa Nahreel sasa baada ya kufika huko sikujua nini kilitokea lakini sikurudishiwa tena kile kitu kilinishangaza kwa sababu Fid ni moja Kati ya wasanii wakubwa sana lakini sina tatizo naye ni kaka yangu tuko fresh”.

Pia Rosa Ree alifunguka kuwa hana muda wa kuwaza mapenzi kwa sasa kwaniyuko bize na kuzisaka pesa kwanza na kuboresha maisha yake.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.