Rosa Ree Awatolea Povu The Industry na Kusema Hawawezi Kumshusha

Mwanamuziki wa Bongo fleva anayetamba kwa miondoko yake ya kurap na hata kupewa jina the rap Godess Rose Kimario ‘Rosa Ree’ amewatolea povu zito wale wote wanaotaka kumshusha hawataweza kushusha kipaji chake kikubwa.

Rosa Ree alipata umaarufu kwa mara ya kwanza baada ya kuwa chini ya uongozi wa The Industry ambao uko chini wa Nahreel na Aikah Navykenzo.

download latest music    

Tangu alipoondoka kwenye label hiyo na kuanza kufanya muziki kama Solo artist Miezi michache iliyopita siku zote amekuwa akisisitiza kuwa hana bifu wala ubaya na Navykenzo.

Lakini siku chache ziliopita Rosa Ree aliibuka na kuongelea mchezo mchafu aliofanyiwa na Uongozi wake wa zamani ambapo amedai wamefuta baadhi ya video za nyimbo zake YouTube ambazo zilikuwa kwenye kurasa yao lakini pia amesema nyingine wamezishusha wameziweka private jambo ambalo amedai limemrudisha nyuma.

Rosa Ree amefanya Interview na Enews ya East Africa Tv amekiri pamoja na kwamba kitendo hiko kimemrudisha nyuma lakini hakijamkatisha tamaa na hakiwezi kushusha kipaji chake:

Kusema ukweli walivyoshusha video zangu kuna thamani ambayo imeshuka kidogo na ninajikongoja kuweza kupita ile sehemu ambayo ilikuwa zinaweza kunifikisha lakini siamini kama video zikishushwa kwenye YouTube na kipaji changu kimeshushwa kwaiyo nina iyo imani kwamba bado kipaji changu kipo na bado uwezo wangu upo na nitaendelea kufanya vyema”.

Pia Rosa Ree aliulizwa kuhusu uhusiano wake na Navy Kenzo kwa sasa endapo kuna bifu lolote ambalo linapelekea wao kumfanyia hivyo yeye na alisema:

Sina mawasiliano yoyote na Navykenzo kwa muda mrefu Lakini naamini ni kwa sababu ya majukumu mimi niko busy na muziki wangu hivyo sijaweza kuwasiliana nao lakini na wao wamepata mtoto ambalo ni jukumu kubwa naamini hivyo siwezi kujiuliza kwa nini hatuwasiliani”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.