Rosa Ree Kufuata Nyayo Za Diamond,Ni Baada Ya Kupata Dili Nono

Msanii anaefanya vizuri kwa sasa katika anga za muziki wa bongo , Rosa Ree amekuwa msanii wa kwanza wa kike lakini wa pili kutoka Tanzania kupata deal kubwa kutoka katika kampuni ya Belaire baada ya Diamond kupata dili hili week chache zilizopita.Kampuni iyo ambayo ina mabalozi wengine wakubwa duniani  kama Rick Ross  inaendelea kuona kazi nzuri wanazofanya wasanii wa Tanzania na kuamua kufanyanao kazi,

Akiongea na mwandishi wa habari msanii Rosa Ree amethibitisha kupata dili ilo na anasema kuwa anahisi ni kwa sababu ya muziki na kazi zake kufanya vizuri ndio maana ameweza kuchaguliwa lakini hajui nini kuliwasukuma kampuni iyo kumuangalia na kumchagua msanii kama yeye ambae ndio kwanza anaibuka na kuanza kufanya vizuri tofauti na Diamond ambae amekuwa katika industry ya muziki kwa muda mrefu kidogo.

download latest music    

To be honest mimi sijui kwa sababu na mimi nimechaguliwa hivyhivyo tu na wao wenyewe hata sikujichagua, au kujipendekeza nikasema labda nina quality sana , kwaio hata ukiniuliza sijui ni quality gani Belaire wanaangalia kuchagua wasanii  na sijui ni zipi waliangalia wakaona Rosa Ree anafaa” alifunguka Rosa Ree

Hata hivyo Rosa Ree anasema kuwa muda mwingine vile unavyojichukulia ndivyo na watu wanaokuangalia watakuchukulia pia kana unakaa kutokujiamini itakuwa hivyo kwa watu pia”lakini najua kwamba ukiweza kujichukulia mwenyewe kwa uzito fulani  na watu wanaweza kukuchukulia kwa uzito huohuo na kwa thamani hiyo na ukijikuta unafika katika viwangi vikubwa” aliongezea mwanadada huyo

Rosa Ree ni msanii chipukizi ambae alianza kazi chini ya lebel ya The industry, hata hivyo kutokana na juhudi zake kwa sasa anafanya kazi vizuri akiwa kama moja wa ma-rapper bora wa kike Tanzania mwenye style ya pekee katika uimbaji,kama ilivyo kwa Diamond, Rosa Ree pia amepata dili la kuwa msanii anatoka Tanzania wa kike atakae kuwa balozi wa kinywaji chenye brand  kubwa duniani cha Belaire.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.