Rose Muhando Kukufuliwa Tena Kwenye Muziki Wa Injili

Rose Muhando ni msanii wa kike wa injili aliyekuwa ameteka nyoyo za waamini wengi sana katika muziki wa injili, sio kwa upande wa kikristo tu lakini Rose alibeba mashabiki katika dini zote  hii yote ni kutokana na vile ambavyo msanii huyo alivyokuwa akifanya vizuri katika muziki wa injili.Imepita muda wa takribani miaka miwili au zaidi tangu msanii huyu wa kike awe kimya katika muziki wa injili, ingawa  kumekuwa na wasnii wengi wanochipukia na wamekuwa wakifanya vizuri lakini bdao kiu ya mashabiki kwa msanii Rose Muhando bado inaonekana.

Akiongea na waandishi wa habari, aliyekuwa meneja wa msanii huyo Alex Msama anasema kuwa ni kweli rose muhando alikuwa kimya kwa muda mrefu lakini hiyo yote ilisababishwa na yeye mwenyewe kwa sababu kuna kipindi alikuwa ameendekeza tabia ya utapeli kwa mashabiki zake na baadahi ya mameneja.Pia kulikuwa na kesi nyingi sana polisi zilikuwa zikimhusu, lakini kwa sasa anampngo wa kumrudisha tena kwa mashabiki ili aendelee kuwaburudisha mashabiki zake kwa sababu kwa sasa msanii huyo maebadilika kabisa na ana imani atafanya vizuri tena kama hapo awali.

download latest music    

  Rose alizidisha sana mambo yake ya utapeli ndio maana nikaacha kufanya nae kazi, na tangu hapo roseamepotea kabisa katika muziki wa injili,lakini nimethamilia kumrudisha hivi karibuni tu  mashabiki na wapenzi wake wakae mkao wa  kula maana rose ni msanii mzuri  sana na anajua kuimba vizuri.-Alisema meneja huyo

Hii itakuwa ni moja ya habari njema kwa mashabiki wa injili kwa sababu nyimbo za Rose Muhando zilikuwa zikipendwa na kuchezwa na watu wa kila rika na kila dini kutokana na uzuri wake.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.