RPC Mbeya Athibitisha Kukamatwa Kwa Uwoya na Wenzake.
Wikiend iliyopita kulisambaa kwa taarifa kuwa msanii Irene Uwoya na Tausi walikamatwa na polisi baada ya kuktwa katika kiwanja kimoja cha starehe muda mabao sio kwa kuendeleza starehe. Hata hivyo taarifa zilikuwa zikisema kuwa wasanii hao walitoka polisi hapo kwa dhamana.
Habari za kuaminika zinasema kuwa ni kweli wasanii hao walikamatwa na hawakuwa wawili tu bali walikuwepo na wengine kama Mtanga na Kupa ambao walikutwa katika kiwanja kimoja wakinywa pombe muda ambao ulikuwa ni wa kufunga.
Hata hivyo mtioa habari anasema kuwa wasanii hao walikamatwa na kulala lupango mpaka siku ya pili jion ambapo mtu mmoja aliejulikana kwa jina la Fadhili anaesemekana kuwa ndio aliwaalika katika shoo jijini Mbeya aliwatoa kwa dhamana na kuachiwa huru
Baada ya hapo GLP Waliamu kumtafuta mhusika kituon hapo ndipo walipoongea na afande matei amabe alikiri na kusema “ni kweli tulimtia mbaroni, Irene, tausi na wenzake hao,walikamatwa na polisi wa doria baada ya kukutwa bar wakiendelea kunywa wakati muda wa kufunga ulikuwa umeshafika, tuliwakamata kwa sababu tukitaka wao pia wao mfano mzuri kwa wengine kwa sababu wao nikioo cha jamii.
lakini tliona hakuna haja ya kulikuza kwa sababu taifa lilikuwa katika masikitiko makubwa ya janga a MV Nyerere, lakini watu watambue kabisa ni marufuku kunywa pombe muda wa kazi au kupituliza muda wa kufunga.