Ruby Adai Wasanii Wengi Wanashindwa KujiBrand

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Ruby amefunguka na kusema sababu kubwa iliyonfanya akae kimya ni ilikua ni kwa dhumuni la kujitengezea au kujibrand kibiashara zaidi.

Msanii huyo ameweka wazi kuwa wasanii wengi wanafeli katika hilo kwani inapelekea wao kushindwa kujitengenezea soko lao binafsi la biashara.

download latest music    

Kama tunavyojua tofauti na zamani hivi sasa muziki ni biashara zamani muziki ulikuwa ni burudani tu lakini sasa watu wanaishi na kuendesha maisha yao kwa kutegemea muziki.

Kwenye Interview na Bongo 5, Ruby alifunguka na kutaka sababu za ukimya wake ambapo aliweka wazi kuwa ni katika kujitengeneza na kumuweka kibiashara zaidi.

Kwa sababu napenda vitu vizuri na vyenye kukaa kwenye biashara yangu muda mrefu kwa sababu nilikuwa natengeneza soko langu binafsi.

Watu wamekosa ile akili ya ziada ya kibiashara kwamba muziki si vile watu wanataka ila ni vile unautengeza kwa sababu ni kitu chanko kila mtu ana biashara yake”.

Baada ya ukimya mrefu tangu aondoke Clouds Fm, hatimaye ameachia wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la Niwaze ambao amewashirikisha kundi la The Mafik.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.