Ruby Afunguka Kuhusu Kushindwa Kufanya Show South Afrika.
Msanii wa muziki wa bongo fleva RUBY ambae alikuwa kimya kwa miaka kadhaa kutokana na matatizo ya manejiment , lakini kwa sasa amerudi tena katika game amefunguka na kujibu tuhuma alizokuwa akizushiwa kwa muda mrefu kuhusu yeye kushindwa kufanya shoo nchini Afrika ya Kusini kwa madai ya kuwa alikuwa amelewa sana kutokana na vitu alivyokuwa akitumia na kumfanya abaki kulala tu hotelini.
Hata hivyo baada ya kuulizwa na eNews kuhusu habari hizo aliwajibu kwa hasira na kuhamaki na huku akisema kuwa habari hizo sio za kweli watu wanaongea vitu visivyokuwa na ukweli ndani yake
“kuna sababu nyingi sana za kusafiri na mimi ukiona nimesafiri ujue nimeenda kupiga kazi , kiufupi ninaweza kusema kuwa watu wa south afrika ni watu peacefully sana , wakisema wanakipend kitu basi ujue wanakipenda kweli na siwezi kusema ni show ngapi nimefanya nikiwa kule ila huwa naziweka katika ukurasa wangu wa instagram.
Ruby alikuwa kimya kwa muda mrefu lakini amerudi sasa na kutoa wimbo aliowashirikisha kundi la The Mafik.