Ruby Aiangukia Clouds FM Kwa Magoti na Kuomba Msamaha

Msanii wa Bongo fleva Ruby Africa amejishusha na kuiangukia kituo cha redio cha Clouds FM baada ya bifu lao la muda mrefu.

Msanii Ruby ambaye alijipstia umaatufu kwa mara ya kwanza alipokuwa chini ya THT (Tanzania House of Talent) aliingia kwenye mgogoro na uongozi wake huo na kusababisha kufarakana hali iliyopelekea Ruby kuendelea kuwa kimuziki kivyake.

download latest music    

Baada ya kutengana na kituo hicho Ruby alipotea kimuziki kwani hakuna nyimbo yake iliyovuma na baadae kuamua kupumzika kufanya sanaa kwa kipindi cha mwaka mzima wa 2017.

Baada ya kutangaza kurudi rasmi kwenye sanaa mwaka huu mwanzoni Ruby alifanya mahojiano na kipindi cha XXL ya Clouds FM kwa kipindi kirefu tangu afarakane nao na alianza kwa kuomba msamaha kwa kituo hiko na mashabiki zake alifunguka yafuatayo:

Ujumbe huu ni kwa yoyote, awe mwanakamati wa Clouds, team clouds au shabiki  wa nje napenda kuomba msamaha na kusema sorry to my fans, sorry to my management Clouds media na pia sorry to my country, Clouds nawapenda sana nisameheni nilikosea ninachohitaji ni support yenu, naamini kwamba ukiwa mjinga kwenye kila kitu ndio utapata kujua vitu vingi sana, nilikaa nikamuomba boss wangu Rugs samahani Mimi ni mdogo wewe ni Mkubwa kwaiyo kwa chochote Mimi nimekosea”.

Tangu alipogombana na uongozi huo wa Clouds Media Group nyimbo zake zilipigwa stop kupigwa na pia alikuwa haalikwi kwenye shoo za Clouds kama Fiesta lakinitangu ameomba msamaha nyimbo zake zimeanza kusikika Clouds.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.