Ruby Ajisifu Kuwa Nandy Mamuwezi Katika Muziki

Ruby ni moja ya wasanii waliokuja na kufanya vizuri sana katika tasnia ya muziki lakini ndoto zake zilizimika baada ya kukosana na menejimenti yake na kushindwa kuendelea na muziki kwa kipindi cha muda mrefu kidogo , lakini moja ya wasanii wa kike wenye kipaji cha kuimba na anaweza kufanya vizuri kama atapewa nafasi nyingine ya kufanya muziki.

Hivi karibuni msanii Ruby amekuja na nyimbo yake mpya iliyokwenda kwa jina la ‘are  you ready’, ambayo ni ya kwanza tangu kukaa kwake kimya kwa kipindi kirefu kidogo.

download latest music    

Aliipoulizwa kuhusu kimya chake cha muda mrefu Ruby aliibu kuwa sababu  moja wapo ya kukaa kimya ni kumpa nafasi msanii mwenzie Nandy ili aweze kujulikana katika muziki kwa sababu endapo na yeye angeendelea kufanya kazi basi Nandy asingeweza kufanya vizuri katika muziki kama ilivyo sasa.

Ruby anasema kuwa ujio wa Nandy haukuksumbua sana kwa sababu ana amini kuwa Nandy ni msanii mzuri lakini hakutaka kuanza kujishindanisha nae,lakini pia anasema kuwa watu wengi wamekuwa wakisema kuwa ujio  wa Nandy ulikuwa ni wa kuziba pengo aliloliacha lakini ukweli ni kwamba yeye na Nandy wote wanafanya muziki wa aina moja lakini bado kuna tofauti kubwa kati yao hasa upande wa TONE  na SCALES zao katika muziki wanaoimba.

Hata hivyo Ruby ameomba kutokushindwanishwa na mtu yoote kwa sababu hapendi kushindana na mtu katikamaisha yake zaidi ya yeye mwenyewe tu, na hata kama wanafanya muziki wa aina moja  haimaanishi kuwa wanafanana hata kidogo.

Ruby anatangaza kurudi tena katika muziki na kusema kuwa wakati yupo kimya alikuwa akiumia sana pale alipokuwa akiona mashabiki zake wanalalamika na kumuomba arudi na kwamba walikuwa wakim-miss sana.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.