Ruby: Nimechoka Kusikia Habari za Nandy Kila Siku

Msanii wa Bongo fleva Ruby amechoshwa na kile alichodai ni kuulizwa habari za Nandy kila siku anapohojiwa.

Ruby na Mwanamuziki mwenziye Nandy wanasemekana kuwa wana bifu la chinichini kwa kile kinachodaiwa wamegombania bwana, ingawa wawili hao wameziki kukana kuwa kila mmoja hana tatizo na mwenziye lakini habari chini ya kapeti zinadai kuwa wawili hao ni panya na paka (hawapatani).

download latest music    

Ruby alifunguka hayo kwenye kwenye mahojiano aliyoyafanya hivi karibuni na stesheni moja ya redio na kudai kuwa amechoshwa na watangazaji wa media mbali mbali badala ya kumuuliza maswali ya maana kila siku wamekalia kumuuliza habari za Nandy ambazo kwa sasa zimeshamchosha na ni kitu kinachotengeneza ugomvi baina yao hata kama hakuna ugomvi.

Nachukia sana swali la kufananishwa na Nandy Kwa sababu honestly I am tired of that question! ni kama vile watangazaji wanashindwa ni maswali gani ya kuuliza , maswali ni yale yale nimeshayajibu sana ! I love Nandy she is a good artist, she is a good singer but don’t ask me too much questions about her, it’s like mnataka kutengeneza ugomvi sasa nashindwa kuelewa hata watu wa media mnatengeneza ugomvi sasa kwasababu swali lilishajibiwa mara Mia moja sasa kwa nini lijirudie kila siku?”.

Nandy na yeye alipoulizwa mara ya mwisho kama ana ugomvi na Ruby alikana kata kata ingawa wambea wa mjini wanadai eti kuwa wawili hao walikuwa marafiki walipokuwa wote THT lakini Ruby alipoondoka tu Nandy akajiweka kwa jamaa/ sponsor wa Ruby hivyo kusababisha ugomvi (habari hazijathibitishwa)

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.