Sababu ya kesi ya Masogange kutosikilizwa mwezi huu

Agnes Gerald anayetambulika kama Masogange bado anangoja kusikilizwa kwa kesi yake baada ya kutofika mahakamani Jana, Julai 13, 2017 kama ilivyohutajika.

Kulingana na wakili wa mrembo huyu, inasemekana kuwa hangeweza kufika kutoka na kuumwa kwa mwili. Wakili wake, Reuben Simwanza akizungumza na hakimu aliomba radhi kwa mteja wake.

download latest music    
Agnes Masogange
Agnes Masogange

Hata hivyo wakili wa Serikali, Constantine Kakula, hakufurahishwa na maneno haya huku akikumbusha mahakamani kuwa hapo mbeleni Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri, alikuwa amepeana amri ya kuwa kesi hiyo ianze kusikilizwa Jana.

Agnes Masogange

Wakili wa Masogange aliweza kuisihi mahakama kuihairisha kesi kesi hiyo hadi July 25, 2017. Masogange hata hivyo ameshtakiwa kwa makosa ya kutumia dawa za kulevya aina ya Heroine na Oxazepam na Heroine.

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua