Saida Karoli ampa staa wa Tottenham – Victor Wanyama zawadi kusherekea siku ya kuzaliwa kwake

Victor Wanyama alizuru Tanzania kwasababu ya mapumziko, kiungo huyo wa Tottenham Hotspur pia alihudhuria shindano la kandanda akiwa nchini humu.

Serikali ya wilaya ya Ubungo ilimpa heshima Victor Wanyama kwa kuipa moja ya barabara za Ubongo jina la nyota huyo ambaye alikuwa mgeni wa heshima kwenye mchezo wa Ndondo Cup 2017 kati ya FC Kauzu dhidi ya Faru Jeuri.

download latest music    

Hata hivyo serikali hio ilibadilisha hatua ya kuipa moja ya barabara jina la Wanyama wakidai kuwa utaratibu haukuzingatiwa.

Hata kama serikali ya wilaya ya Ubungo ilifuta jina la Wanyama kwa barabara, staa huyo wa Tottenham alipata zawadi nzuri kutoka wa Saida Karoli.

Wawili hao (Wanyama na Karoli) walikutana kwenye studio za Clouds FM na Wanyama alimjulisha Karoli kuwa yeye ni shabiki wake mkuu.

Na kwa bahati nzuri siku waliokuta ilikua birthday ya Wanyama ambaye alikua anatimia umri wa 26; Karoli alimpa Wanyama CDs zake kama zawadi.

“Thank you @saidakarolitz for the CDs,I’m humbled,” Wanyama aliandika.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere