Salamu Za Wasanii Kutoka kwa Ney Wa Mitego

Akiwa ni mmoja kati ya wasanii wanaofanya vizuri katika tasnia hii ya muziki, mwanamuziki wa Bongo Fleva Emmanuel Elibariki  Ney Wa Mitego  “True Boy” ameamua kuwashauri wasanii wenzie wanaokaa kimya kwa muda mrefu  bila kutoa nyimbo huku wakitegemea kuwa watakapotoa  watapokelewa vizuri na mashabiki zao.

Ney wa mitego ameyaongea maneno hayo alipokuwa kwenye mahojiano  na kituo cha  Televisheni Cha Taifa ‘Tbc’ katika kipindi cha Papaso , Ney Wa Mitego  anasema kuwa kwa sasa game la muziki limebadilika  sana hivyo si vizuri kwa wasnii  kukaa kwa muda mrefu bila kutoa wimbo kama walikuwa wamezoa hapo mwanzo.

download latest music    

“huo muda umeisha, this time mtu akirudia hivyo basi tenaa!!yaani tunamsahahu kabisa, game hilo halipo tena”alisema Ney Wa Mitego.

Kwa muda  sasa   kumekuwa na tabia za mazoea  kwa   baadhi wasanii wa muziki  kukaa  kimya kwa muda mrefu sana  bila kutoa nyimbo  mpya wamekuwa  wakisahau kabisa  kuwa wanafanya baadhi ya mashabiki  wao kuwa na kiu na kuchoka kusubiri kwa muda mrefu, hata hivyo kutoa nyimbo kila baada ya muda pia kunafanya kukua kwa muziki.

Hata hivyo, katika maneno hayo aliyosema  Ney wa Mitego hakuonesha kumlenga msanii yoyote  ingawa ni kawaida kwa baadhi ya  wasanii wakubwa wa muziki kukaa kimya mpaka mashabiki zao wanaanza kurushiania maneno katika mitandao huku wakimuuliza anatoa lini nyimbo mpya. Kama msanii  alikiba ni mmoja wa wasanii wenye  tabia ya kukaa kimya kwa muda mrefu bila kutoa nyimbo, hivyo kama msanii   Ney Wa Mitego ametaka anajaribu kuwahasa wasanii wenye tabia hizo   kuacha  kwa sababu game la muziki  limebadilika watafikiri mashabiki wanawasubiri kumbe ndo wanawapoteza mashabiki.

Ney Wa Mitego ni moja kati ya wasani ambao nyimbo zao zinapendwa na mashabiki kwa sababu uongea ukweli katika mashairi yake bila kuogopa, mara nyingi amejikuta hata akiingia katika majibizano na baadhi ya wasanii wenzie kwa sababu ya kusema ukweli wao. Kwa sasa anatamba na kibao chake kinachokwenda kwa jina la “Makuzi’

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.