“Sasa aliokwambia namtaka Damond ni nani? Wema Sepetu awaonya mashabiki dhidi ya kumhusisha na Diamond Platnumz

Wema Sepetu amesisitiza kuwa uhusiano wake wa kimapenzi na Diamond Platnumz ulikamilika kabisa. Mwigizaji huyo wa filamu ya Bongo amesema anataka mume bora.

Wema na Diamond walikua wapenzi kabla ya mwimbaji huyo kumtema Wema na nafasi yake kuchukuliwa na Zari Hassan.

download latest music    

Mara nyingi watu husema kuwa Wema na Diamond bado wako na uhusiano wa kimapenzi ila wanachezea chini ya maji mapenzi yao isigunduliwe.

Diamond and Wema Sepetu

Wema amesisitiza kuwa yeye na Diamond hawana lolote tena, alisema hayo wakati akimjibu shabiki katika kurasa wake wa Instagram.

“Sasa baby aliokwambia namtaka Damond ni nani? Life has to go on, yule ni baba wa watoto wawili jamani. Its about time u guys accept that me and Naseeb no more. Mnachotakiwa kuniombea ni nipate mwanaume bora na siyo bora mwanaume na mwenye heshima zake,” aliandika Wema Sepetu Instagram.

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere