Sauti Ya Ruby Yaacha Historia Tuzo Za SZIFF

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Hellen George maarufu kama Ruby ameacha historia ya aina yake kwenye tuzo za SZIFF Baada ya kupiga bonge la shoo.

Ruby ameweka historia Jumamosi ya Februari 23, 2019 kwenye kumbukumbu za wapenda burudani wengi, achana na namna waigizaji wachanga walivyowaangusha mastaa kwenye kipengele cha Muigizaji bora wa kike na wakiume, bali namna shoo kali kutoka kwa msanii Rubby alikonga nyoyo za mamia waliofika kuhudhuria hafla hiyo ya kipekee kwenye Ukumbi wa Mlimani City jijini.

download latest music    

Rubby ambaye alipanda kwenye jukwaa la SZIFF saa 4:50 hadi saa 5:13 usiku aliamsha shangwe la maana baada ya kutoa burudani ambayo haikuacha chembe yoyote ya shaka, achilia mbali vazi lake kali.

Mashabiki mbali mbali walishindwa kujizuia na kumimiminika stejini kwa ajili ya kumtunza ambapo anasemekana kupata pesa nyingi sana.

Lakini pia mastaa mbali mbali kama Jokate Mwegelo, Mama Diamond na wengineo wamempongeza Ruby na kuisifia sauti yake matata.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.