Seven Mosha Ataja Ugonjwa Unaomsumbua Ommy Dimpoz

Meneja wa msanii wa Bongo fleva Omary Nyembo maarufu kama Ommy Dimpoz, Seven Mosha amefunguka kuhsuu ugonjwa ambao umekuwa ukimsumbua Msanii huyo.

Ommy Dimpoz aliweka wazi ugonjwa wake kwa mara ya kwanza Miezi miwili iliyopita ambapo alitangaza kuwa alifanyiwa operesheni.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Millard Ayo Tv, Seven Mosha amefunguka na kusema Ommy bado yupo nje ya nchi ambapo anaendelea na matibabu:

Ugonjwa uliokuwa unamsumbua ni koo yaani Esophagus ambayo ilikuwa inampa shida kupitisha chakula halafu baadae hata kupitisha kinywaji chochote kwaiyo ilibidi atengenezewe mfumo mpya”.

Lakini pia Seven amesema hivi sasa Ommy anaendelea vizuri ingawa bado yupo nje ya nchi ambapo anaendelea na matibabu:

Bado yupo nje ya nchi hospitali ambapo anaendelea na check-up kwa sababu ilikuwa ni operesheni kubwa sana lakini tu nashukuru Mungu anaendelea vizuri na bila Shaka mwisho wa wiki hii ataweza kurudi kufanya kazi kama kawaida”.

Seven ameweka wazi pia operesheni aliyofanyiwa haitaathiri uimbaji wake hata kidogo tofauti na maneno ambayo yamekuwa yakisemwa Kwenye vyombo vya habari.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.