Shamsa Ford Adai Hajali Kuchukiwa na Watu Ilimradi Anapendwa na Mumewe

Msanii wa filamu za kibongo Shamsa Ford amefunguka na kusema hajali kama watu  watamchukia kwa muonekano wake au hata kusema ukweli inapobidi ilimradi anapendwa na mume wake Chidi Mapenzi inatosha.

Shamsa amekuwa Kwenye headlines za mitandao ya kijamii tangu avae gauni lililokuwa fupi sana Kwenye arobaini ya mtoto wa Zamaradi Mketema wiki iliyopita.

download latest music    

Kwenye mahojiano na gazeti  Amani baada ya watu wengi kumshambulia kwenye mitandao ya kijamii kutokana na kutokelezea na nguo fupi kwenye 40 ya mtoto wa Zamaradi, na kusema kuwa ni ngumu kumridhisha kila mtu kwenye maamuzi yako.

Mimi Mungu kanijalia maneno sijali kabisa na isitoshe Chidi akinipenda na akakubaliana na maamuzi yangu kwangu inatosha kabisa siwezi kumridhisha kila mtu”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.