Shamsa Ford: Mwanamke Mwingine Hatosababisha Nimuache Mume Wangu

Mwigizaji wa Bongo movie Shamsa Ford amefunguka na kudai kuwa kamwe hatokaa amuache mume wake Chiddi Mapenzi kwasababu ya yeye kuwa na mwanamke mwingine.

Katika siku chache zilizopita kumekuwa na tetesi za wawili hao waliooana miezi michache iliyopita kuachana kutokana na kukosekana kwa uaminifu baina yao baada ya tuhuma za Chiddi kuwa na uhusiano na wanawake wengine nje ya ndoa.

download latest music    

Kwa kupitia ukurasa wake wa Instagram Shamsa alifunguka haya;

“Nakupenda mume wangu halali wa ndoa aliyenipa Mwenyezi Mungu. Sitoachana na wewe Kisa makelele ya wanadamu, nitaachana na wewe kwa mapenzi ya Mwenyezi Mungu. Unanipenda, unaniheshimu, unajishusha kuomba msamaha pale unapokosea  wakati wanaume wengine hawawezi kuomba msamaha hata wakikosea. Mume wangu nikikuelewa mimi inatosha wengine wakipiga kelele tuchukulie kama burudani tu. Maana anajitahidi huyo anayeitwa ILALA MJINGA kama ulivyomsave kwenye simu yako kusambaza msg kwenye magroup na kuwatumia waandishi ushahidi, jamani sitokaa nimuache mume wangu kwaajili ya mwanamke hata siku moja labda afanye makubwa yasiyoeleweka kwenye jamii. Amecheat Bill Clinton sembuse Rashid wangu? Nakupenda Rashid wa Shamsa Ford tupambane tuzidi tujenge familia yetu”.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.