ShiiKANE- Diamond ni Msanii Anayejituma Hata Kama Humpendi, Utakubali Kazi Zake

Kundi la muziki kutoka Nigeria linaloundwa na wadada watatu wanaojulikana kama ShiiKANE wamefunguka na kumkingia kifua staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Miezi michache iliyopita Diamond alishinda tuzo ya msanii bora wa kuime nchini Nigeria na kuwabwaga mastaa wakubwa kama Davido kitendo ambacho kiliwakera Wanigeria ambao waliweka wazi kuwa hawakupenda Diamond kushinda.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Bongo 5, Kundi hilo la ShiiKANE kutoka Nigeria linasema Diamond alistahili tuzo hiyo kutokana na ukweli usiopingika kuwa ni mchapakazi na kazi zake ni nzuri.

Ni mtu anayejituma hata kama haupendi au kupenda muziki wake lazima ukubaliane na anachikifanya kwa sababu anastahili kushinda alichokishinda. Kila utakapomuongea basi jua ndivyo anavyozidi kuwa juu”.

Katika tuzo hizo Diamond alishinda katika kipengele cha Best Male MVP na kuwabwaga wasanii kama Runtown, Davido, Olamide, 2face Idibia, Wizkid, Shatta Wale, Navio na Sarkodie.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.