ShiiKANE- Tunatamani Kufanya Kazi na Diamond Lakini Ali Kiba Kwanza

Mastaa wa muziki kutoka Nigeria ShiiKANE wamefunguka na kuweka wazi kuwa wanatamani sana kufanya kazi na Diamond lakini mpaka wakishafanya kazi na Ali Kiba Kwanza.

Wasanii hao watatu wanaounda kundi hilo la ShiiKANE wapo nchini Tanzania kutoka nchini Nigeria kwa ajili ya kufanya kazi na baadhi ya wasanii wa nchini hapa Lakini pia kwa ajili ya kutangaza muziki wao.

download latest music    

Wasanii hao wamekiri kuwa wanatamani kufanya kazi na wasanii wa Bongo Diamond na Ali Kiba lakini mmoja wa wadada wa kundi hilo Shay amekiri kuwa wanataka kufanya kazi na Ali Kiba kwanza.

Wasanii hao walifunguka hayo Kwenye mahojiano waliofanya na Bongo 5:

Tunatamani kufanya kazi na mtu kama Diamond ila kwanza Alikiba kisha Diamond ila tayari tumesha fanya kazi na Chin Bees ambaye ametufundisha Kiswahili kidogo katika kazi tuliyofanya“.

Lakini pia mbali na Diamond na Ali Kiba ShiiKANE wamesema Msanii wanaye ramani kufanya naye kazi ni Vanessa Mdee kwani wamekiri wanavutiwa na kazi zake sauti  yake na hata urembo wake.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.