Shilole Amchana Barakah The Prince, Huku Mx Cater Adai Ana Stress

Mwanamuziki wa Bongo fleva, Barakah the Prince amezidi kuwa katika kipindi kigumu wiki hizi chache tangu atoe wimbo wake mpya ‘sometimes’.

Tangu ametoa wimbo huo, Barakah amekuwa katika headline baada ya kudai kuwa label yake ya zamani Rockstar 4000 na Mx Cater wanamfanyia hila ili nyimbo yake mpya isivume wala kupata viewers YouTube.

download latest music    

Mapema wiki iliyopita Barakah alidai kuwa MX cater ambaye ni meneja wa wanamuziki Aslay na Shetta alimuomba password ya akaunti yake mpya ya YouTube kwa lengo la kumfanyia uchunguzi wa nani anamfanyia mchezo huo mchafu, lakini Barakah anadai baada ya kumuamini na kumpa password hali ile ikaanza kutokea tena kwenye akaunti yake mpya.

Barakah amedai kuwa habari za yeye kufanyiwa mchezo mchafu na MX carter amepewa na msanii mwenzake Shilole, jambo ambalo Shilole amelikataa kwa nguvu zote ambapo amedai kuwa Barakah ni muongo na mchonganishi.

Lakini kwa nini huyu mtoto anapenda kugombanisha watu? Na ndio maana haelewani na watu kwa sababu ya mambo yake anayoyafanya siyo vizuri kama unataka kuongea na mtu mfuate binafsi si mpaka upitie kwa mtu mwingine, yaani sikipendi nasema ukweli halafu yule ni mdogo wangu namheshimu, yule mtoto ajipange unajua sometimes unataka kiki lakini siyo za namna hiyo, ana dharau sana yule mtoto nasema hiyo dharau haitampeleka kokote, kwangu mimi hapati kiki bali nitamuharibia sitoi kiki kishenzi”.

Pia Shilole amezidi kusisitiza kuwa hajawahi kumwambia Barakah jambo kama hilo mara ya mwisho waliongea kwenye Simu ambapo Barakah alimuomba ampostie Nyimbo yake mpya, lakini pia Baada ya tuhuma hizo MX cater alikataa tuhuma hizo alizopewa na Barakah kudai Ana stress za nyimbo yake mpya kufeli.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.