Shilole Athibitisha Kuhamia Kwenye Mjengo Wake Wa Thamani

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole amefunguka na kuweka wazi kuwa amehamia kwenye mjengo wake mpya uliopo Majohe jijini Dar-Es-Salaam.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la DIMBA, Shilole alisema kuwa anashukuru Mungu kuona baadhi ya mipango yake kwa mwaka huu ikitimia ikiwa ni pamoja na kuhamia kwenye nyumba hiyo ya kisasa.

download latest music    

Katika interview hiyo Shilole alitakiwa kumtaka thamani ya Nyumba lakini alishikwa na kigugumizi na kusema hapendi kuweka wazi hilo.

Kikubwa ni kwamba nakaa kwenye nyumba yangu, hilo ndilo la kumshukuru Mungu, ukiniuliza nimetumia kiasi gani siwezi kukujibu kwa haraka kwa kuwa kama unavyojua pesa zetu za mawazo na nilikuwa nahanga ikanikipata kidogo naweka mpaka nilivyofika hapa“.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.