Shilole Awatolea Uvivu Wasanii Ambao Hawamuungi Mkono Raisi

Mwanamuziki wa Bongo fleva Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole amewajia Juu wasanii wenzake ambao hawakujitokeza kumuunga mkono Raisi katika uzinduzi wa treni mpya leo.

Kwenye mahojiano aliyofanya na waandishi wa habari siku ya jana kwenye tukio la wasanii kutembelea mradi wa SGR, amesema kuwa wasanii wawe kitu kimoja kwa kumsapoti Rais Magufuli kwa vitu anavyovifanya.

download latest music    

Unajua unavyojichanganya na wenzio ndio unavyopata connections. Mtu ambaye anaitwa na kiongozi wako halafu hautii, hiyo sio heshima, it means huwezi kuheshimu wazazi wako. Unajua unavyoitwa na Rais huwezi jua anakuitia nini?je, akikuteua kuwa mkuu wa mkoa, au mkuu wa Wilaya utakataa”.

Lakini pia Shilole amemtumia maombi Raisi ili aweze kumpa tenda ya kwenda kuuza chakula:

Kwanza nataka nimuombe ombi Mhe. Rais Magufuli, nataka aniruhusu niuze chakula kwenye Treni itakapoanza kazi, mimi sitaki hela nataka tu anipe nafasi hiyo basi“.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.