Shilole Aweka Wazi Siri Ya Mafanikio Yake

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole amefunguka na kuweka wazi Siri iliyompa mafanikio makubwa.

Mbali tu ya kuwa msanii wa Bongo fleva na kutoa nyimbo kali kama Chuna Buzi, Nyang’anyang’a, Kigori, Hatutoi Kiki, Malele, Nakomaa na Jiji, Say My Name, Paka la Baa na nyinginezo Lakini pia Shilole ni mjasiriamali.

download latest music    

Shilole ambaye alianza safari yake ya Sanaa kwenye kuigiza filamu za Kibongo na kutoa kazi kali kama vile Fair Decision’, ‘Crazy Of Love’, ‘Pigo’, ‘Bed Rest’, ‘Cut Off’ na nyinginezo Lakini pia Shilole anamiliki mgahawa unaoitwa Shishifood.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Shilole amefunguka kuhusu kufungua kampuni yake ya Shilole Entertainment:

Nilianza biashara zangu na mtaji wa shilingi 50,000 tu mpaka hapa mnaponiona nimefikia kwa sasa, japo haikuwa rahisi kama mnavyodhani kwa sababu walikuwepo walionisema vibaya kwamba sitafika popote, wakunikatisha tamaa walikuwa wengi lakini namshukuru Mungu kwa kuwa maneno yao hayakufanikiwa.

Nilihakikisha napambana kadri niwezavyo ili nifikie malengo yangu, nashukuru leo hii wote waliokuwa wananisema vibaya wanayaona mafanikio”.

Lakini pia Shilole alizidi kufunguka zaidi na kuanika Siri ya mafanikio yake:

Namshukuru Mungu ninaendelea vizuri na biashara zangu, nikiendesha maisha yangu bila kumtegemea mtu yeyote, hivyo nawashauri na wengine ambao wana ndoto yakuja kuwa wajasiriamli wakubwa, kwanza kabisa wasikate tamaa waamini katika malengo yao na pia waanze biashara na kidogo walichonacho siyo mpaka wawe na mtaji mkubwa mwisho wa siku watayaona mafanikio”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.